Muheza, Tanga
Naibu Wazir wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega jana Julai 01, 2020 ametembelea Vyama vya Ushirika wa Wafugaji wa ng'ombe wa maziwa katika wilaya ya Muheza mkoani Tanga.
Naibu Waziri Ulega katika ziara hiyo alikabidhi vibebea maziwa (cans) 50 kwa Chama Kikuu cha wafugaji Mkoani Tanga (TDCU) kwa ajili ya ubebaji maziwa.
![]() |
Naibu Wazir wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akikabidhi vibebea maziwa (cans) 50 kwa Wanaushirika wa Chama Kikuu cha wafugaji Mkoani Tanga (TDCU) kwa ajili ya ubebaji maziwa |
Cans hizo zimetolewa na Marafiki wa Maendeleo, Heifer International kupitia program zake kusaidia ukusanyaji wa maziwa kutoka kwa vyama vya msingi vya wafugaji hadi kiwandani Tanga Fresh Ltd kwa Usindikaji ambapo cans hizi zitagawanya kwa vyama vya msingi wanachama wa TDCU.
Aidha, Naibu Waziri Ulega alikabidhi pia gari la kubebea maziwa kwa TDCU ambalo litasaidia kubeba maziwa ya wafugaji. Gari hilo kwa sasa litakuwa katika kituo cha Muheza na lingine linatarajia kufika mwezi Novemba,2020.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi na wanachama wa Vyama vya Ushirika wa Maziwa mkoani Tanga.
Naibu Waziri Ulega pia katika ziara hiyo alikuja kujua kuhusu mafanikio na changamoto za mkopo wa TADB kwa mkoa wa Tanga kwa kuwa mkoa huo ndio ulikuwa wa majaribio (pilot) kwa mikopo ya TADB kwa Sekta ya Ufugaji. Kutokana na changamoto alizoelezwa, Mhe. Ulega alielekeza Wataalam wa Sekta Binafsi kukaa na TADB kutoa mwelekeo wa nini kifanyike kwa Mfugaji.
No comments:
Post a Comment