Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (wapili kushoto) akiongea kwenye Kikao na Viongozi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Wakulima wa Bonde la Bahi |
Wito
huo umetolewa wakati wa Kikao na viongozi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Wakulima
wa zao la Mpunga wa Bonde la Bahi, Jumanne Juni03, 2020 alipokuwa katika ziara
ya kikazi Wilayani Bahi, mkoani Dodoma.
Naibu
Waziri amesema kuwa Serikali ina dhamira ya dhati ya kumuinua mkulima ili
anufaike na kilimo chake. Hivyo, ni vyema wakulima kutumia mifumo ya Ushirika
pamoja na vituo vya ukusanyaji mazao katika maeneo yao kwaajili ya urahisi wa
kufikisha mazao yao katika maghala ya uuzaji kwaajili ya kupata bei yenye tija
itakayopatikana kupitia minada rasmi.
Wanaushirika wa Skimu ya Umwagiliaji ya Wakulima wa zao la Mpunga wa Bonde la Bahi wakiwa katika mkutano na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe |
Wanaushirika wa Skimu ya Umwagiliaji ya Wakulima wa zao la Mpunga wa Bonde la Bahi wakiongea na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe |
“Tunaweza
kuamua kuhifadhi kwenye ghala gunia mbili za mazao ya mkulima hiki kikiwa ni
wastani wa kwa kiwango cha chini na kwa pamoja tukaamua kuyauza mazao hayo kwa
mnada wa uwazi ambapo mapato yatakayopatikana yatusaidie wenyewe kuimarisha
kilimo chetu,” alisisitiza Bashe.
Katika
Kikao hicho Naibu Waziri amewaagiza Viongozi wa Wilaya na Halmashauri ya Bahi
kutenga maeneo maalum ya uuzaji wa mazao ya wakulima wadogowadogo ili kuwa na
urahisi kukutana na wauzaji katika hatua za soko la awali, akisisitiza maeneo
hayo kuwa na mizani zilizokaguliwa ili wakulima wauze kwa vipimo sahihi na si
vinginevyo.
Wanaushirika wa Skimu ya Umwagiliaji ya Wakulima wa zao la Mpunga wa Bonde la Bahi wakiandaa mazao yao kwaajili ya huhifadhi na kuuza |
Mhe. Bashe
amewataka Viongozi wa Skimu, Viongozi wa Wilaya ya Bahi kushirikiana kwa pamoja
na Wadau wa maendeleo pamoja na taasisi za kifedha kuangalia namna bora ya
kuongeza thamani ya mpunga huo kwa kuanzisha kiwanda chenye kinu cha kukoboa mpunga na hatimaye kuuza mchele.
Jambo ambalo wakulima hao waliliunga mkono kutokana na kuongeza ubora wa
thamani na kuongeza kipato kwa wakulima.
Pamoja
na mambo mengine, Naibu Waziri ameagiza Watendaji wa Wilaya ya Bahi kwa
kushirikiana na Serikali kuratibu zoezi
la kuwatambua wakulima kwa lengo la kuanzisha kanzidata ya wakulima pamoja na
upatikanaji wa vitambulisho kwa wakulima wa Bonde la mpunga la Bahi. Akifafanua
kuwa Skimu hiyo ikawa ni mfano utakaoendelezwa katika maeneo mengine ili
kuongeza tija na ufanisi kwa wakulima.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amemshukuru Naibu
Waziri wa Kilimo kwa kufika katika Wilaya hiyo kuona shughuli mbalimbali za
Kilimo zinazoendelea Wilayani hapo. Mkuu huyo alipongeza juhudi zinazoendelea
hususani za uimarishaji wa Ushirika kwa mfumo wa Stakabadhi ya ghala ambao
unaendelea kutekelezwa Wilayani hapo kipindi hiki ambapo minada ya mazao
ikiendelea na wananchi wakinufaika na bei za mauzo za minada hiyo.
No comments:
Post a Comment